Monday, September 28, 2015

MAJERUHI YA VIUNGO WA KUKABA YAMTIA MAWAZO WENGER.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger anaweza kufanya mabadiliko katika safu yake ya kiungo ya kukaba wakati kikosi chake kitakapokabiliana na Olimpiakos katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya kesho. Katika mchezo huo Arsenal itawakosa nyota wake Mathieu Flamini na Mikel Arteta lakini wakati Francis Coquelin akiwa ameanza mazoezi baada ya kupona majeruhi ya goti, Wenger amekiri kuwa hajaamua kama nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 atakuwa fiti kwa ajili ya kucheza. Akihojiwa kuelekea katika mchezo huo leo, Wenger anafahamu kuwa Coquelin ameanza mazoezi lakini bado anamfuatilia kwa karibu kama atafaa kucheza kesho. Arsenal inatafuta ushindi wake wa kwanza katika michuano hiyo baada ya kutandikwa mabao 2-1 na Dinamo Zagreb mapema mwezi huu.

No comments:

Post a Comment