Monday, September 28, 2015

TIMU ZA MISRI MDEBWEDO MICHUANO YA KOMBE LA SHIRIKISHO.

KLABU ya Etoile du Sahel ya Tunisia jana imefanikiwa kupiga hatua moja kuelekea fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho baada ya kuwatandika mabingwa mara mbili Zamalek. Mahasimu wa Zamalek nchini Misri, Al Ahly nao pia waliambulia kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Orlando Pirates ya Afrika Kusini katika mchezo uliofanyika huko Soweto. Al Ahly wana faida ya kucheza nyumbani katika mchezo wao wa marudiano utakaofanyika Jumapili ijayo huko Suez wakati Zamalek nao wataikaribisha Etoile Jumamosi jijini Cairo. Mechi za mikondo miwili za fainali ya michuano hiyo zimepangwa kuchezwa Novemba 20 au 22 huku marudiano ikiwa wiki moja baadae.

No comments:

Post a Comment