Tuesday, September 29, 2015

BLATTER ACHOMOA KUJIUZULU.

RAIS wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Sepp Blatter amesema hawezi kuachia wadhifa huo kwasababu ya mashitaka ya uhalifu yaliyofunguliwa dhidi yake na wachunguzi nchini Uswisi. Blatter mwenye umri wa miaka 79, anatuhumiwa kwa kusaini mkataba usiokuwa na manufaa kwa FIFA na kufanya malipo yasiokubalika kwa rais wa Shirikisho la Soka la Ulaya-UEFA Michel Platini. Blatter ambaye anatarajiwa kuachia ngazi nafasi hiyo ifikapo Februari mwakani amesema kuwa hajafanya kosa lolote kinyume na sheria. Platini mwenye umri wa miaka 60, ameandika barua kwa wanachama wa UEFA akikana kufanya kosa lolote. Katika taarifa iliotolewa na mawakili wake, Blatter amesema kuwa pauni milioni 1.5 zilizotolewa kama malipo kwa Platini, ambaye ndio kiongozi wa UEFA mwaka 2011 ni halali na hakuna zaidi.

No comments:

Post a Comment