Tuesday, September 29, 2015

MASCHERANO ASHITAKIWA KWA KUKWEPA KODI.

MAHAKAMA moja nchini Hispania, imemfungulia mashitaka mawili ya ukwepaji kodi kwa kiungo mahiri wa Barcelona Javier Mascherano. Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina anatuhumiwa kushindwa kuweka hadharani kiasi cha euro milioni 1.5 mwaka 2011 na 2012 alizopata kupitia haki za matangazo ya picha yake na kutoa haki hiyo kwa kampuni anazomiliki nchini Ureno na Marekani na kuzitoza kodi za upendeleo. Jalada hilo pia limethibitisha Mascherano alitoa pungufu ya euro milioni 1.75 kwa mamlaka za kodi Septemba 9 mwaka huu ili kulipa kiasi anachodaiwa pamoja na riba. Mascherano anakuwa mchezaji wa pili kutuhumiwa na masuala ya ukwepaji kodi nchini Hispania baada ya Lionel Messi na baba yake kusimama kuzimani mwaka 2013 kujibu mashitaka kama hayo.

No comments:

Post a Comment