Friday, September 25, 2015

PELE AMFUNDA DIEGO COSTA.

NGULI wa soka wa Brazil, Pele amesema tabia aliyoonyesha mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa katika mchezo dhidi ya Arsenal wiki iliyopita inatoa taswira mbaya kwa soka na kupeleka ujumbe mbaya kwa watoto. Pele alitoa kauli hiyo katika shughuli ya maonyesho ya sanaa jijini London kuelekea kusherekea miaka 75 ya kuzaliwa kwake. Nguli huyo alikaririwa na gazeti la Daily Telegraph akidai kuwa tukio la Costa halitoi ujumbe mzuri kwa watoto na sio nzuri kwa mchezo wa soka lakini ni kosa moja. Pele pia aliongeza kuwa angeweza kucheza soka Ulaya badala ya kubakia Santos karibu miaka yake yote ya soka kwasababu siku hizi sio mchezaji anayeamua ni wakala wake. Pele anatarajiwa kutimiza umri wa miaka 75, Octoba mwaka huu.

No comments:

Post a Comment