Friday, September 25, 2015

RODGERS KIKAANGONI LIVERPOOL.

BEKI wa zamani wa Liverpool, Mark Lawrenson amedai kuwa siku kumi zijazo zitakuwa ngumu kwa meneja Brendan Rodgers. Liverpool ilipata ushindi wa matuta 3-2 dhidi ya klabu ya daraja la pili ya Carslisle, baada ya timu hizo kwenda sare katika muda wa kawaida kwenye mchezo wa Kombe la Ligi. Klabu hiyo katika siku 10 zijazo inakabiliwa na michezo miwili ya Ligi Kuu dhidi ya Aston Villa na Everton na Lawrenson amesema Rodgers yuko katika hatari kubwa huku kikosi chake kikikosa hamasa. Lawrenson aliendelea kudai kuwa hapendi kuona mameneja wakitimuliwa lakini kwa mwenendo wa Liverpool sio siri kibarua cha kinaweza kuwa shakani kama asipofanya vyema katika mechi zake zijazo. Naye Rodgers akihojiwa amedai kuwa hatishwi na minong’ono kwamba kibarua chake kiko shakani yeye anachotizama ni kufanya kazi yake kwa ufasaha ili kikosi chake kipate matokeo mazuri.

No comments:

Post a Comment