Friday, September 25, 2015

NUSU FAINALI YA LIGI YA MABINGWA AFRIKA KUANZA KUTIMUA VUMBI KESHO.


MICHUANO ya Ligi ya Mabingwa ya Afrika inatarajiwa kuendelea mwishoni mwa wiki hii kwa mechi za mkondo wa kwanza za nusu fainali kuanza kutimua vumbi. Kesho vigogo wa soka wa Sudan Al Merreikh wataikaribisha TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo-DRC. Mazembe ambao ni mabingwa mara nne wa michuano hiyo, walipata nafasi hiyo kwa kumaliza wakiwa vinara wa kundi A wakati wenzake Al Merreikh wao walimaliza katika nafasi ya pili nyuma ya ASM Alger katika kundi B. Mchezo huo utakuwa ni nafasi kwa kocha wa Al Merreikh Diego Garzitto kukutana tena na klabu yake ya zamani ambayo aliiongoza kunyakuwa taji la michuano hiyo mwaka 2009. Mara baada ya mchezo huo wa kesho timu hizo zitarudiana tena jijini Lubumbashi Octoba 2 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment