Wednesday, September 23, 2015

WAKALA WA POGBA AMJIBU FERGUSON.

WAKALA wa kiungo Paul Pogba, Mino Raiola amejibu vijembe kutoka kwa Sir Alex Ferguson akisisitiza kuwa meneja huyo wa zamani wa Manchester United hajui asemalo. Meneja huyo nguli ambaye alistaafu mwaka 2013 baada ya kuingoza United kwa mafanikio, alimlaumu wakala huyo kuwa ndio chanzo cha kuondoka kwa Pogba kwenda Juventus miaka mitatu iliyopita katika kitabu chake kipya. Raiola amejibu madai hayo akidai Ferguson hawezi kuelewa kuwa uamuzi alioufanya ni kwa faida ya nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa ambaye aliondoka United akiwa mchezaji huru mwaka 2012 lakini sasa thamani yake imepanda mpaka kufikia euro milioni 100. Wakala huyo aliendelea kudai kuwa maneno ya Ferguson hayaharibu kazi yake kwani yeye anayachukulia kama mfano wa jinsi gani anavyofanya kibarua chake vyema. Raiola amesema kazi kuwa ya wakala ni kufanya kilicho bora kwa maslahi ya wachezaji wake na kama angekuwa anafanya kwa maslahi yake Pogba angekuwa United mpaka leo.

No comments:

Post a Comment