Wednesday, September 23, 2015

LEWANDOWSKI AUSHANGAZA ULIMWENGU KWA KUPIGA MABAO MATANO NDANI YA DAKIKA TISA.

MSHAMBULIAJI wa Bayern Munich, Robert Lewandowski jana ameweka rekodi ya kipekee Bundesliga kwa kufunga mabao matano ndani ya dakika tisa katika mchezo dhidi ya Vfl Wolfsburg. Katika mchezo huo Bayern walikuwa nyuma kwa bao 1-0 mpaka muda wa mapumziko, wakati Lewandowski alipoingia kuchukua nafasi ya Thiago. Dakika sita baadae, mchezaji huyo wa kimataifa wa Poland alifunga bao lake la kwanza katika dakika ya 51 kabla ya kuongeza mengine manne dakika za 52, 55, 57 na 60. Ushindi huo umeifanya Bayern kukwea kileleni mwa msimamo wa Bundesliga wakitofautiana kwa alama tatu na mahasimu wao Borussia Dortmund ambao leo wanaivaa Hoffenheim.

No comments:

Post a Comment