Wednesday, September 23, 2015

IBRAHIMOVIC AANZA TAMBO BAADA YA KUFUNGA.

MSHAMBULIAJI nyota wa Paris Saint-Germain-PSG, Zlatan Ibrahimovic amesema atahitaji muda zaidi wa kucheza mara kwa mara kama anataka kurejea katika kiwango chake bora. Nyota huyo wa kimataifa wa Sweden, mwenye umri wa miaka 33, amekuwa akikosolewa kufuatia kuanza msimu akiwa katika kiwango cha chini. Majeruhi tayari yamemfanya kukosa michezo minne ya ligi lakini baada ya kupona na kupata nafasi alifunga bao lake la kwanza jana katika ushindi wa mabao 3-0 waliopata PSg dhidi ya Guinamp. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo, Ibrahimovic amesema anashukuru kwasababu ameanza kurejea katika kiwango chake taratibu ingawa bado anahitaji mechi nyingi zaidi ili arejee katika ubora wake. PSG wanatarajiwa kusafiri kuifuata Nantes Jumamosi hii kabla ya kuifuata Shakhtar Donetsk katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya wiki ijayo.

No comments:

Post a Comment