Wednesday, September 23, 2015

RAFINHA AICHOMOLEA BRAZIL.

BEKI wa Bayern Munich, Rafinha amekataa wito wa kwenda katika kikosi cha timu ya taifa ya Brazil ambacho kinakabiliwa na mechi za kufuzu michuano ya Kombe la Dunia 2018, baadae mwezi ujao. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 30 alikuwa akitarajiwa kuiwakilisha nchi yake kwa mara ya kwanza toka Machi mwaka 2014, wakati kocha wa zamani Luiz Felipe Scolari alipomjumuisha katika kikosi ambacho kilipamban ana Afrika Kusini jijini Johanessburg. Sambamba na nyota wa Real Madrid Danilo na Dani Alves wa Barcelona, Rafinha alipata nafasi ya kuita kwa mara ya kwanza na kocha wa sasa Dunga wiki iliyopita huku akionekana kufurahia wito huo. Lakini beki huyo wa zamani wa klabu za Schalke na Genoa alilishangaza Shirikisho la Soka la Brazil-CBF kwa kugeuka ghafla na kukataa wito huo hivyo hatakuwepo katika mechi dhidi ya Chile na Venezuela. Rafinha alifafanua kuwa sio mchezaji tegemeo sana kwa nchi yake kwani kuna wachezaji wengine wanaoweza kucheza nafasi yake vyema ndio maana ameamua kukataa wito huo ili kuongeza nguvu zaidi kwa klabu yake.

No comments:

Post a Comment