Friday, September 25, 2015

WENGER AKIRI KUMTUMIA MAPEMA SANCHEZ.


MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amekiri Alexis Sanchez ameanza taratibu msimu huu lakini amesisitiza kiwango cha nyota huyo wa kimataifa wa Chile kitaimarika. Mshambuliaji huyo wa zamani wa Barcelona aliisaidia kwa kiasi kikubwa Arsenal msimu uliopita akifunga mabao 25 lilikiwemo moja katika mchezo wa fainali ya Kombe la FA ambao walishinda mabao 4-0 dhidi ya Aston Villa. Baada ya kuisaidia Chile kupata mafanikio katika michuano ya Copa America iliyofanyika kwao majira ya kiangazi, Sanchez amekuwa akisuasua kurejea katika kiwango chake toka kuanza kwa msimu huu. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 26 mpaka sasa hajafunga bao lolote pamoja na kuwa mchezaji aliyepiga mashuti mengi kuliko mchezaji yeyote wa Ligi Kuu. Akihojiwa kuhusiana na hilo Wenger alikiri Sanchez kutokuwa katika kiwango chake lakini alimtetea akidai kuwa alimtumia mapema na anaamin taratibu atarejea katika ubora wake uliozoeleka.

No comments:

Post a Comment