Friday, October 23, 2015

COSTA KUENDELEA KUCHEZA UNDAVA.

MSHAMBULIAJI wa Chelsea, Diego Costa amedai kuwa anafahamu yeye sio malaika pindi awapo uwanjani na hatabadilika aina yake ya uchezaji wa kutumia nguvu. Costa amefungwa mara mbili kutocheza mechi tatu baada ya kumkanyaga mchezaji wa Liverpool Emre Can na baadae kumpiga kibao beki wa Arsenal Laurent Koscielny. Akihojiwa nyota huyo wa kimataifa wa Hispania aliyezaliwa Brazil mwenye umri wa miaka 27, amesema amefikia hapo alipo kutokana na jinsi anavyocheza hivyo hawezi kubadilika kwasababu watu wanataka hivyo. Costa alihamia Stamford Bridge Julai mwaka 2014 akitokea Atletico Madrid na kuisaidia Chelsea kushinda taji la Ligi Kuu na Kombe la Ligi msimu uliopita. Meneja wa Manchester City Manuel Pellegrini amemtaka Costa kupunguza mchezo wake wa kutumia nguvu sana, wakati meneja wa Arsenal Arsene Wenger akimtuhumu mshambuliaji huyo siku kujihusisha na vurugu.

No comments:

Post a Comment