Friday, October 23, 2015

WENGER AMSHUSHUA VAN GAAL.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema atalia kama mechi za Ligi Kuu zitasimamishwa kupisha mapumziko ya sikukuu za Chrismass na mwaka mpya. Arsenal watacheza mechi saba kati ya Desemba 13 mpaka Januari 16, ikiwemo michezo mitatu ndani ya siku saba mwezi Desemba. Akihojiwa kuhusiana na suala hilo Wenger hiyo imekuwa sehemu y utamaduni wa soka la Uingereza hivyo anapenda kuendelea nao. Meneja wa Manchester United Louis van Gaal ameuita utaratibu huyo wakutotoa mapumziko katika kipindi hicho kama utamaduni wa kikatili. Kauli ambayo imepingwa vikali na Wenger akidai kuwa utamaduni huo umekuwa ukilitangaza soka la Uingereza kwani mashabiki wengi Ulaya wamekuwa wakienda kutizama wakati wa kipindi hicho. Ligi za Hispania, Italia, Ufaransa na Ujerumani zote husimamishwa kwa muda kupisha kipindi hicho cha mapumziko.

No comments:

Post a Comment