Thursday, October 22, 2015

MAJANGA YA MAJERUHI YAZIDI KUMUANDAMA RIBERY.

WINGA mahiri wa Bayern Munich, Franck Ribery amepata majeruhi mengine tena baada ya kushindwa kuendelea na mazoezi leo. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 32 hajacheza mechi yeyote toka Machi mwaka jana ikiwa ni matokeo ya majeruhi ya kifundo cha mguu aliyopata katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Shakhtar Donetsk msimu uliopita. Mwezi uliopita ofisa mkuu wa Bayern, Karl-Heinz Rummenigge alidai kuwa Ribery anaweza kurejea tena uwanjani kabla ya kumalizika kwa mwaka huu. Lakini kutokana na na leo kundolewa mazoezini zikiwa zimepita dakika 17 kuna uwezekano mkubwa wa winga huyo mkongwe wa kuendelea kukaa nje kwa kipindi kirefu zaidi.

No comments:

Post a Comment