Thursday, October 22, 2015

CELTIC YALINASA JEMBE LA ZAMANI LA WEST HAM.

KLABU ya Celtic imefanikiwa kumsajili mshambuliaji wa zamani wa kimataifa wa Uingereza Carlton Cole kwa mkataba utakaomalizika mwaka 2017. Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 32 alikuwa mchezaji huru na amekuwa akifanya mazoezi na klabu ya Parkhead kwa wiki kadhaa baada ya kuondoka West Ham United. Cole amefunga mabao 85 katika mechi zaidi ya 380 za klabu alizocheza zikiwemo Chelsea, Wolves, Charlton, Aston Villa na West Ham. Mkongwe huyo ametambulishwa rasmi katika mkutano na wanahabari uliofanyika mapema leo jijini Glasgow.

No comments:

Post a Comment