Thursday, October 22, 2015

WALES KUCHEZA NA UHOLANZI KIRAFIKI.

TIMU ya taifa ya Wales inatarajiwa kuanza maandalizi yake ya michuano ya Euro 2016 kwa kucheza mechi ya kimataifa ya kirafiki dhidi ya Uholanzi ambao wameshindwa kufuzu michuano hiyo. Mchezo huo unatarajiwa kufanyika Novemba 13 mwaka huu katika Uwanja wa Cardiff City uliopo jijini Cardiff. Wakati Wales wakisheherekea kufuzu michuano hiyo kwa mara ya kwanza baada ya kupita miongo kadhaa hali ni tofauti kwa Uholanzi ambao wameshindwa kufanya hivyo kwa kumaliza wakiwa nafasi ya nne katika kundi lao. Timu hizo zitakwaana kwa mara ya kwanza toka Juni mwaka 2014 wakati Uholanzi walipoichapa Wales mabao 2-0 katika maandalizi ya Kombe la Dunia nchini Brazil mchezo uliofanyika jijini Amsterdam.

No comments:

Post a Comment