Thursday, October 22, 2015

DYNAMO KIEV YAINGIA TENA 18 ZA UEFA.

SHIRIKISHO la Soka la Ulaya-UEFA limefungua kesi ya kinidhamu dhidi ya klabu ya Dynamo Kiev kutokana na vurugu zilizofanywa na mashabiki wake na mambo ya kibaguzi katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Chelsea jana. Katika mchezo huo uliofanyika katika mji mkuu wa Ukraine Chelsea waliambulia sare ya bila kufungana. Matokeo hayo ynaifanya Chelsea kubaki katika nafasi ya tatu katika kundi G wakiwa alama moja nyuma ya Dynamo. Katika taarifa yake UEFA imesema itaanza kusikiliza kesi hiyo Octoba 27 mwaka huu. Hiyo sio mara ya kwanza kwa mashabiki wa timu hiyo kuinia matatani kwani msimu uliopita Dynamo walitozwa faini ya kufungiwa upande mmoja wa uwanja kwa makosa mawili mojawapo likiwa vurugu na lingine ubaguzi katika mchezo wa Europa League.

No comments:

Post a Comment