Thursday, October 22, 2015

CRUYFF AGUNDULIKA NA SARATANI YA MAPAFU.

TAARIFA kutoka nchini Hispania zimedai kuwa nguli wa soka wa Uholanzi, Johan Cruyff amegundulika kuwa na saratani ya mapafu. Vyombo vya habari vikiwemo vile vya radio na magazeti vimeripoti kuwa nguli huyo mwenye umri wa miaka 68 aligundilika na maradhi hayo Jumanne na kwasasa anaendelea kufanyiwa vipimo kujua ukubwa wa tatizo linalomkabili. Cruyff aliisaidia timu yake ya taifa ya Uholanzi kufika hatua ya fainali ya michuano ya Kombe la Dunia mwaka 1974. Nguli huyo pia amewahi kushinda mataji matatu ya Kombe la Ulaya akiwa na klabu ya Ajax Amsterdam na baadae kwenda kucheza na kuifundisha Barcelona. Akiwa kocha wa Barcelona alifanikiwa kuisaidia kushinda taji lao la kwanza la Kombe la Ulaya mwaka 1992 na Kombe la Washindi la Ulaya mwaka 1989.

No comments:

Post a Comment