Thursday, October 22, 2015

SARE DHIDI YA MADRID YAMPA KIBURI MENEJA WA PSG.

KUFUATIA Paris Saint-Germain-PSG kupata sare ya bila kufungana na Real Madrid katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya jana, meneja wake Laurent Blanc anaamini kikosi chake kina uwezo wa kupata mafanikio zaidi msimu huu. Blanc aliingoza PSG kushinda mataji matatu ya ndani msimu uliopita na Blanc bado ana uhakika kikosi chake kina ubora wa kupata mataji zaidi msimu huu. Kocha huyo amesema siri kubwa ya kuwa na kikosi imara kinacheza kwa umoja ni kutofanya mabadiliko makubwa kwa mwaka jambo ambalo walilifanya ndio maana anaamini wanaweza kufanya vizuri. Sare hiyo waliyopata jana imezifanya timu hizo kufungana alama katika kundi A kabla ya kuendelea katika mchezo wao marudiano wiki mbili zijazo.

No comments:

Post a Comment