Wednesday, October 21, 2015

RAMSEY PANCHA TENA.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema kiungo wa kimataifa wa Wales Aaron Ramsey amekuwa na huzuni baada ya kupata majeruhi mengine ya msuli wa paja.Ramsey mwenye umri wa miaka 24, alitolewa katika kipindi cha pili katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya ambao Arsenal iliifunga Bayern Munich mabao 2-0 jana.Wenger amesema Ramsey anatarajiwa kuukosa mchezo wa Ligi Kuu Jumamosi hii dhidi ya Everton na anaweza kuendelea kuwa nje ya uwanja kwa muda.Kocha huyo aliendelea kudai kuwa nyota huyo amemwambia kuwa amehuzunishwa na kuumia kwake lakini ameahidi kurejea akiwa imara zaidi.Majeruhi ya msuli wa paja yamekuwa yakimsumbua Ramsey mara kwa mara kwani msimu uliopita pekee aliwahi kukaa nje ya uwanja kwa vipindi vitatu tofauti.

No comments:

Post a Comment