Wednesday, October 21, 2015

NEYMAR AIONGOZA BARCELONA KUINYUKA BATE.

MSHAMBULIAJI wa Barcelona, Neymar kwa mara nyingine ameonyesha uwezo wa kuongoza na kusiba nafasi ya Lionel Messi kufuatia ushindi waliopata dhidi ya BATE Borislov katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya.Huku Messi akiwa nje kwa miezi miwili kutokana na majeruhi ya goti majukumu yameangukia kwa Neymar kuiongoza Barcelona katika safu ya ushambuliaji jambo ambalo amekuwa akilifanya vyema.Jumamosi iliyopita Neymar alifunga mabao manne katika ushindi mnono wa La Liga waliopata dhidi ya Rayo Vallecano na jana alifanikiwa kutoa pasi zote mbili za mwisho za mabao yaliyofungwa na Ivan Rakitic katika ushindi wa mabao 2-0 waliopata dhidi ya BATE.Beki wa Barcelona, Marc Bartra alimsifia mshambuliaji huyo akidai amekuwa akifanya vyema katika kutengeneza mashambulizi kama anavyofanya Messi.

No comments:

Post a Comment