Wednesday, October 21, 2015

MASHABIKI WA BAYERN WAANDAMANA KUPINGA UGHALI WA TIKETI.

KUNDI la mashabiki wa Bayern Munich waliingia uwanjani wakiwa wamechelewa katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya uliofanyika katika Uwanja wa Emirates, wakipinga bei kubwa ya tiketi katika mchezo huo.Kundi hilo ambalo lilibainisha maandamano yao wiki iliyopita, hawakuingia uwanjani kwa dakika tano za kwanza za mchezo huo ambao tiketi zake zilipatikana kwa paundi 64.Mashabiki wa Bayern pia walionyesha mabango yaliyokuwa yakisomeka kwa maandishi makubwa kupinga bei hiyo waliouziwa tiketi.Meneja wa Bayern, Pep Guardiola amesema atazungumza na meneja wa Arsenal, Arsene Wenger ili katika mchezo ujao waweze kufanya tiketi rahisi kwa mashabiki wao.Arsenal ilishinda mabao 2-0 katika mchezo wa jana na watarudiana tena Novemba 4 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment