Wednesday, October 21, 2015

ROONEY ATAMBA KUENDELEA KUNG’AA PAMOJA NA UMRI KUMTUPA MKONO.

NYOTA wa Manchester United, Wayne Rooney ana uhakika bado ana miaka mingi mbele yake ya kucheza soka pamoja na kujiandaa kusheherekea miaka 30 ya siku yake ya kuzaliwa Jumamosi hii.Nahodha huyo wa United na timu ya taifa ya Uingereza tayari yuko katika msimu wake wa 14 katika Ligi Kuu toka alipoibuka kwa mara ya kwanza katika kikosi cha Everton akiwa na miaka 16 mwaka 2002.Akihojiwa Rooney amesema kimwili bado anajisikia vyema na pamoja na umri aliokuwa nao sasa lakini bado anajiona mdogo katika soka hivyo anaweza kucheza kwa miaka mingi ijayo.Nyota huyo amesema anashukuru kwa kutokuwa na majeruhi makubwa makubwa hivyo kumpa nafasi ya kuwa na uwezo wa kuendelea kuchza kwa kipindi kirefu zaidi.

No comments:

Post a Comment