Wednesday, October 21, 2015

MOURINHO KAMA KAWAIDA YAKE ALIA NA MWAMUZI BAADA YA SARE.

MENEJA wa Chelsea, Jose Mourinho amemfananisha mwamuzi aliyechezesha mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya ambao walitoka sare ya bila ya kufungana na Dynamo Kiev, na mwamuzi waliyechezesha mchezo wa Kombe la Dunia la Raga kati ya Scotland na Australia.Mwamuzi Craig Joubert wa Afrika Kusini alikosolewa vikali baada ya kuizawadia penati Australia katika dakika za laa salama katika mchezo wa robo fainali dhidi ya Scotland jana.Mourinho alimshambulia mwamuzi Damir Skomina kwa kuwanyima penati wakati Cesc Frabregas alipofanyiwa faulo katika eneo la hatari.Kocha huyo amesema kama mwamuzi huyo angewapa penati hiyo hali ya mchezo ingebadilika lakini hakufanya hivyo.Chelsea inashika nafasi ya tatu katika kundi G wakiwa na alama nne katika michezo mitatu waliyocheza, alama tatu nyuma ya vinara FC Porto.

No comments:

Post a Comment