Wednesday, October 21, 2015

TOURE AWAPASHA WACHEZAJI WENZAKE.

KIUNGO mahiri wa Manchester City, Yaya Toure amesema hawatakuwa na chakujitetea kama wakishindwa kunyakuwa taji lolote msimu huu baada ya kuimarisha kikosi chao kwa kusajili wachezaji kadhaa wakubwa majira ya kiangazi.City walifanikiwa kuwasajili Raheem Sterling, Kevin De Bruyne na Nicolas Otamendi wakijaribu kuimarisha kikosi chao kufuatia kutoka kapa bila taji msimu wa 2014-2015.Na Toure sasa amesema hawatakuwa na sababu msimu huu, kwani mafanikio ndio jukumu lao kuu baada ya kikosi kuimarishwa vyema.Toure amesema kwa kipindi kirefu wamekuwa katika kivuli cha Manchester United lakini sasa ni wakati wao wa kutoka huko na kuonyesha dunia kuwa wanaweza.City ambao wanaongoza Ligi Kuu kwa tofauti ya alama mbili dhidi ya Arsenal wanaoshka nafasi ya pili, watakuwa wenyeji wa Sevilla katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya baadae leo.

No comments:

Post a Comment