Wednesday, October 21, 2015

LAMAR ODOM ARUHUSIWA KUJIUGUZA NYUMBANI.

MCHEZAJI nyota wa zamani wa Ligi ya Mpira wa Kikapu nchini Marekani-NBA, Lamar Odom amerejeshwa jijini Los Angeles baada ya kupatiwa matibabu katika hospitali huko Las Vegas, wiki moja baada ya kukutwa hajitambui katika danguro huko Nevada.Katika taarifa iliyotolewa na familia yake Odom ataendelea kujiuguza Los Angeles na amedaiwa kupona kwa haraka kwani ameshaanza kutembea kidogo kidogo.Mke wake ambaye walikuwa mbioni kuachana Khloe Kardashian, baba yake na watoto wake wawili wote wako pamoja na mkongwe aliyekuwa akicheza katika timu ya Los Angeles Lakers.Odom ambaye alimuoa Kardashian nyota wa vipindi vya luninga mwaka 2009, amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya matumizi ya dawa za kulevya kwa kipindi kirefu.Polisi bado wanaendelea kufanyia uchunguzi vipimo ili kubaini haswa kilichotokea kabla ya kukumbwa na tukio hilo.

No comments:

Post a Comment