Wednesday, October 21, 2015

WENGER AANZA KUCHONGA BAADA YA KUICHAPA BAYERN.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema ushindi dhidi ya Bayern Munich utaongeza imani katika Uwanja wa Emirates.Arsenal ilipoteza mechi zake mbili za mwanzo za Ligi ya Mabingwa lakini mabao ya Olivier Giroud na Mesut Ozil yameifanya timu hiyo kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Bayern jana.Klabu hiyo ambayo bado inashikilia mkia katika kundi F inatarajiwa kupambana tena na Bayern Novemba 4 mwaka huu.Wenger amesema ilikuwa muhimu kushinda mchezo huo na wamefanya hivyo wakiwa chini ya shinikizo kubwa jambo ambalo litaimarisha imani yao na imani ya mashabiki wao.

No comments:

Post a Comment