Sunday, October 18, 2015

PSG IKO TAYARI KUPAMBANA NA MADRID - IBRAHIMOVIC.

MSHAMBULIAJI nyota wa Paris Saint-Germain-PSG, Zlatan Ibrahimovic amewaonya Real Madrid kuwa wako tayari kwa ajili yao baada ya kufunga mara mbili katika ushindi wa mabao 2-0 waliopata dhidi ya Bastia. Mabao yote yalipatikana katika dakika 20 za mwisho katika mchezo huo uliofanyika jana ambao umeifanya PSG kuendelea kukaa kilele mwa msimamo wa Ligue 1 kwa tofauti ya alama tano. PSG inayonolewa na Laurent Blanc sasa wanakuwa hawajafungwa katika mechi 10 za ligi huku pia wakishinda mechi zao mbili za kwanza za Ligi ya Mabingwa Ulaya. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Ibrahimovic amesema matokeo waliyopata ni mazuri kwani wameifunga timu ngumu kwani mara ya mwisho waliondoka wakiwa wamefungwa mabao 4-2. Nyota huyo aliendelea kudai kuwa sasa wanahamishia nguvu zao katika mchezo dhidi ya Madrid ambao watakuwa nyumbani na ni matumaini yao watapata matokeo wanayohitaji.


No comments:

Post a Comment