Sunday, October 18, 2015

USHINDI DHIDI YA EVERTON WAMPA JEURI VAN GAAL KUELEKEA MCHEZO WAO DHIDI YA CITY.

MENEJA wa Manchester United, Louis van Gaal amesema kikosi chake kinaweza kujumuishwa katika kinyang’anyiro cha ubingwa wa Ligi Kuu kama wakifanikiwa kuwafunga mahasimu wao Manchester City Jumapili ijayo. United jana ilifanikiwa kuifunga Everton kwa mabao 3-0 wakati vinara wa ligi City wakiicharaza Bournemouth kwa mabao 5-1 katika Uwanja wa Etihad. Akihojiwa Van Gaal amesema siku zote lengo lao limekuwa ni ubingwa na wataweza kuingia katika kinyang’anyiro hicho kama wakifanikiwa kuifunga City katika mchezo wao ujao. Kocha huyo alikuwa akitaka kikosi chake kurejea katika kiwango chao baada ya kufungwa na Arsenal mabao 3-0 kabla ya mapumziko kupisha mechi za kimataifa na mabao mawili ya mapema waliyopata jana yalifanya ushindi wao kuwa rahisi. Van Gaal aliwapongeza wachezaji wake kwa kiwango kizuri walichoonyesha katika mchezo huo na anadhani kuwa huo ni mwanzo wa ushindi katika mechi zingine zitakazofuata.

No comments:

Post a Comment