Sunday, October 18, 2015

WALCOTT ADAI ARSENAL IKO TAYARI KWA AJILI YA BAYERN.

MSHAMBULIAJI wa Arsenal, Theo Walcott anaamini wanaweza kuifunga Bayern Munich kama wakifanikiwa kucheza kwa kiwango cha juu katika ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Manchester United. Arsenal waliishangaza United kwa kuonyesha soka maridadi la kushambulia na kufuatiwa na ushindi mwingine wa mabao 3-0 dhidi ya Watford katika mchezo wa Ligi Kuu uliochezwa jana. Timu hiyo sasa inakabiliwa na mchezo mwingine wa hatua ya makundi ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Bayern ambapo watakuwa wakihitaji alama tatu muhimu baada ya kushindwa kupata alama yeyote katika mechi zao mbili za kwanza. Akihojiwa Walcott amesema kucheza dhidi ya bayern kwa kiwango walichonacho hivi sasa itakuwa changamoto kwao lakini wakiwa nyumbani na mashabiki wao watahitaji kucheza kwa kiwango cha juu kama walivyofanya dhidi ya United. Nyota huyo aliendelea kudai kuwa wanafahamu kuwa wanaweza kumfunga yeyote na watakwenda katika mchezo huo wakiwa tayari.

No comments:

Post a Comment