Sunday, October 18, 2015

KLOPP AMKINGIA KIFUA ORIGI.

MENEJA wa Liverpool, Jurgen Klopp anaamini Divock Origi anaweza kupunguza tatizo la majeruhi katika safu ya ushambuliaji wa klabu hiyo baada ya kuanza katika mchezo wake wa kwanza wa Ligi Kuu jana walipotoa sare ya bila kufungana na Tottenham Hotspurs. Nyota huyo wa kimataifa wa Ubelgiji mwenye umri wa miaka 20 ndiye aliyekuwa mshambuliaji kiongozi katika kikosi kilichoitwa na Klopp katika mechi yake ya kwanza akiwa Liverpool baada ya kuchukua na Brendan Rodgers aliyetimuliwa. Mapema katika kipindi cha kwanza Origi alipiga kichwa safi kilichogonga mwamba kabla ya kupotea mchezoni lakini Klopp amesema chipukizi huyo atacheza vyema akipata uzoefu na kubainisha alitaka kumsajili kutoka Lille wakati akiinoa Borussia Dortmund. Klopp amesema alitaka kumchukua Origi wakati akiwa Dortmund lakini aliwahiwa na Liverpool ambao baadae walimrudisha kwa mkopo hukohuko Lille. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa Origi ni mchezaji mzuri mwenye kasi na ufundi mzuri, kwasasa anapungukiwa na suala la uzoefu kwasababu hajapata nafasi ya kucheza mara kwa mara ila ana uhakika ataimarika vyema.

No comments:

Post a Comment