Sunday, October 18, 2015

PELLEGRINI AWAMWAGIA SIFA STERLING NA BONY.

MENEJA wa Manchester City, Manuel Pellegrini amepongeza muunganiko wa Raheem Sterling na Wilfried Bony kwani wawili wameonyesha wanaweza kuziba nafasi ya Sergio Aguero na David Silva waliokuwa majeruhi. Sterling alicheza kama mshambuliaji wa kati na kufunga hat-trick, wakati Bony naye akifunga mabao mawili katika ushindi wa mabao 5-1 walioupata dhidi ya Bournemouth jana. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo, Pellegrini amesema walilazimika kufanya kitu tofauti wakiwa bila Aguero na Silva. Aguero na Silva pia wanatarajiwa kuuukosa mchezo wa Jumapili ijayo dhidi ya Manchester United kutokana na majeruhi yanayowasumbua. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa anashukuru kwasababu alimbadilisha Sterling nafasi kwa kumchezxesha katikati huku Bony akiwa mbele yake na mbinu yake hiyo kufanikiwa kwa kiasi kikubwa.

No comments:

Post a Comment