Sunday, October 18, 2015

RONALDO RASMI AIPITA REKODI YA RAUL.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Ureno, Cristiano Ronaldo amefanikiwa rasmi kuwa mfungaji bora wa wakati wote wa Real Madrid kufuatia kufunga bao katika ushindi waliopata dhidi ya Levante jana. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 30 alifunga bao lake la 324 katika La Liga kwenye mechi 310 alizocheza na kuipita rekodi iliyowekwa na nguli wa zamani wa klabu hiyo Raul. Madrid tayari walikuwa wakitambua rekodi hiyo ya Ronaldo, wakimpa bao ambalo lilimgonga Pepe mwaka 2010. Mwaka huo Ronaldo alipiga mpira wa adhabu ambao ulimgonga Pepe na kutinga wavuni na La Liga kuhesabu bao hilo kuwa la Pepe lakini Madrid wao waking’ang’ania kuwa ni la mshambuliaji huyo. Hata hivyo kwa bao alilofunga jana inamfanya Ronaldo rasmi kuivunja rekodi hiyo hata kama ukiliondoa bao hilo moja.

No comments:

Post a Comment