Sunday, October 18, 2015

NEYMAR APIGA NNE BARCELONA IKICHARAZA VALLECANO.

MSHAMBULIAJI nyota wa Barcelona, Neymar jana alifanikiwa kufunga mabao manne yakiwemo mawili ya penati wakati walipoitandika Rayo Vallecano na kuwafanya kulinga alama katika msimamo wa La Liga na vinara Real Madrid. Barcelona walifanikiwa kutoka nyuma kufuatia kufungwa bao la mapema na Javi Guerra na kupata ushindi huo wa pili katika michezo yao minne iliyopita. Faulo alizofanyiwa Neymar katika eneo la hatari zilimfanya kufunga mabao mawili kwa penati katika kipindi cha kwanza kabla ya kuongeza mengine mawili kipindi cha pili na Luis Suarez kufunga lingine katika dakika za majeruhi katika ushindi wa mabao 5-1. Neymar mwenye umri wa miaka 23 sasa anakuwa amefikisha mabao nane msimu huu na kumfanya kuwa mfungaji anayeongoza La Liga.  Hata hivyo, pongezi nyingi zinapaswa kumuendea mlinda mlango wa barcelona Claudio Bravo ambaye aliokoa michomo mingi ya hatari kutoka kwa Vallecano.

No comments:

Post a Comment