Friday, October 23, 2015

MOROCCO, TUNISIA ZAFUZU CHAN.

TIMU ya taifa ya Morocco imefanikiwa kuichapa Libya kwa mabao 4-0 jana katika mchezo wa kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani-CHAN Ukanda wa Kaskazini. Ushindi huo umewafanya kufuzu kwa pamoja na Tunisia michuano hiyo itakayofanyika nchini Rwanda mwakani. Libya walikuwa wakihitaji ushindi katika mchezo huo ili waweze kuwa na nafasi ya kusonga mbele kufuatia kuifunga Tunisia kwa bao 1-0 Jumatatu iliyopita. Morocco ndio wamesonga mbele wakiwa vinara wa kundi lao kwa alama saba wakifuatiwa na Tunisia walioshika nafasi ya pili kwa kuwa na alama nne.

No comments:

Post a Comment