Friday, December 18, 2015

BENZEMA AMEKOSEA - DESCHAMPS.

KOCHA wa timu ya taifa ya Ufaransa, Didier Deschamps amesema Karim Benzema alifanya makosa juu ya sakata la mkanda wa ngono na hataweza kuitumikia nchi hiyo katika michuano ya Euro 2016 mpaka jina lake litakaposafishwa. Mshambuliaji huyo wa Real Madrid anakabiliwa na makosa ya jinai baada ya kutuhumiwa kuhusika katika sakata hilo ambalo linamhusu mhchezaji mwenzake Mathieu Valbuena. Akihojiwa kuhusiana na suala hilo Deschamps amesema kwasasa ni jambo lisilowezekana kwa nyota huyo kuitumikia timu ya taifa mpaka pale jina lake litakapotakasika. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa Benzema hajakubaliana na hali ilivyo ndio anadhani amefanya makosa.

No comments:

Post a Comment