Friday, December 18, 2015

DEL BOSQUE KUIACHA HISPANIA BAADA YA EURO 2016.

KOCHA wa timu ya taifa ya Hispania, Vicente del Bosque anategemea kuachia nafasi yake hiyo baada ya michuano ya Euro 2016. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 64 ameliongoza taifa hilo kunyakuwa mataji mawili ya Ulaya pamoja na Kombe la Dunia. Del Bosque ambaye amewahi kuinoa Madrid amesisitiza michuano hiyo itakayofanyika nchini Ufaransa inaweza kuwa ya mwisho kwake na ana matumaini ya kuondoka kwa mafanikio. Akihojiwa kocha huyo amesema kama kila kitu kikienda kama anavyotegemea baada ya michuano hiyo ataachia kibarua chake hicho.

No comments:

Post a Comment