Friday, December 18, 2015

RONALDO AANZA KUWAZA MAISHA BAADA YA SOKA.

MSHAMBULIAJI nyota wa Real Madrid Cristiano Ronaldo tayari ameshaanza kuangazia maisha yake baada ya soka kufuatia kubainisha mpango wake wa kuwekeza zaidi ya dola milioni 40 kwa ajili ya ujenzi wa hoteli za kifahari zitakazokuwa na jina lake CR7 nchini kwake Ureno, Madrid na New York. Akihojiwa Ronaldo amesema wachezaji wengi wa soka wanamaliza kucheza wakiwa hawajui kitu gani wanataka kufanya lakini kwake hilo ni tofauti kwani anataka kuendelea kulilinda jina lake. Ronaldo ambaye ni mshindi wa tuzo tatu za Ballon d’Or ataungana na kampuni inayomiliki hoteli za Pestana ambayo kama ilivyo yeye mmiliki wake pia anatoka Madeira. Nyota huyo amesema akiwa na umri wa miaka 30 sasa ana machaguo mengi na anafurahia kwasababu ana watu wengi wanaomuunga mkono. Ronaldo aliendelea kudai kuwa anataka jina lake kuendelea kuwa bora katika kitu chochote atakachofanya baada ya kuacha soka.

No comments:

Post a Comment