Sunday, December 20, 2015

PIGO ARSENAL, WELBECK MPAKA FEBRUARI.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema mshambuliaji wake Danny Welbeck hatarejea uwanjani hivi karibuni kufuatia upasuaji wake wa goti kusogeza mbele tena. Welbeck amekuwa nje ya uwanja toka Aprili mwaka huu na Wenger anadhani nyota huyo ataweza kurejea uwanjani tena Februari mwaka huu. Mara ya mwisho Wenger alidai kuwa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uingereza mwenye umri wa miaka 25 angeweza kurejea uwanjani Septemba kabla ya kusogeza mbele mpaka Christmas. Hata hivyo akihojiwa leo, Wenger amesema bado Welbeck hataweza kurejea uwanjani hivi karibuni na hilo ni pigo kubwa kwao kwani wanashindwa kuwapa muda wa kupumzika wachezaji wengine.

No comments:

Post a Comment