Thursday, January 21, 2016

REAL MADRID NDIO KLABU TAJIRI ZAIDI DUNIANI, MAN UNITED YAPOROMOKA.

KLABU ya Real Madrid imetajwa kuwa klabu tajiri zaidi duniani kwa msimu wa 11 mfululizo, wakati Manchester United imeporomoka kutoka nafasi ya pili walipokuwepo mpaka nafasi ya tatu na Barcelona kuchukua nafasi ya pili. Klabu ya Paris Saint-Germain-PSG wao wamekwea kwa nafasi moja mpaka nafasi ya nne wakichukua nafasi ya Bayern Munich walioshuka mpaka nafasi ya tano. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na The Deloitte Money League 2016, imedai kuwa klabu zote tano kwa pamoja zimetengeneza kiasi cha paundi bilioni tano katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita. Madrid wao wanaongoza kwa kutengeneza kiasi cha paundi milioni 439 wakifiatiwa na mahasimu wao Barcelona waliotengeneza paundi milioni 426 huku Manchester United wakiwepo nafasi ya tatu kwa kutengeneza kiasi cha paundi milioni 392.

No comments:

Post a Comment