Thursday, January 21, 2016

RANIERI AJIVUNIA REKODI PAMOJA NA KUTOLEWA NA FA.


MENEJA wa Leicester City, Claudio Ranieri amedai kuridhishwa na rekodi nzuri waliyonayo dhidi ya Tottenham Hotspurs msimu huu baada ya kuondolewa katika michuano ya Kombe la FA jana usiku. Leicester walishindwa kutamba mbele ya Spurs na kujikuta wakichapwa mabao 2-0 na kuondolewa katika mzunguko wa tatu wa michuano hiyo. Akihojiwa Ranieri amesema ni miaka 10 Spurs wamekuwa wakijenga timu yao ili kufikia nafasi ya kushiriki michuano ya Europa League na Ligi ya Mabingwa. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa hali ni tofauti kwa upande wao kwani ndio kwanza wameanza safari yao na tayari wanashindana nao. Ranieri amesema ni hatua nzuri kwani katika mechi nne walizokutana na Spurs wameshinda moja, kupoteza moja na kutoa sare mbili.

No comments:

Post a Comment