Thursday, January 21, 2016

OZIL, SANCHEZ FITI KUIVAA CHELSEA.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amedai kuwa nyota wake Alexis sanchez na Mesut ozil wako fiti tayari kwa ajili ya mchezo dhidi ya Chelsea Jumapili hii. Vinara hao wa Ligi Kuu wamekuwa bila ya Sanchez ambaye amefunga mabao sita msimu huu, toka Novemba mwaka jana baada ya kupata majeruhi ya msuli wa paja. Kwa upande wa Ozil yeye alikosa mchezo wa ligi uliopita dhidi ya Stoke City uliomalizka kwa sare ya bila kufungana, baada ya kusumbuliwa na majeruhi ya kidole gumba. Akihojiwa Wenger amesema ana habari njema kwani Sanchez na Ozil watakuwepo katika mchezo huo muhimu. Wenger aliendelea kudai kuwa kiungo Francis Coquelin amerejea katika mazoezi kamili toka aumie katika mchezo dhidi ya West Bromwich Albion Novemba mwaka jana wakati Danny Welbeck ambaye hajacheza msimu huu naye akitarajiwa kuanza mazoezi wiki ijayo.

No comments:

Post a Comment