Thursday, January 21, 2016

LIVERPOOL YAJITOSA KWA TEIXEIRA.

KLABU ya Liverpool imejitosa rasmi katika mbio za kumsajili mshambuliaji wa Shakhtar Donetsk Alex Teixeira. Taarifa zinadai kuwa meneja wa Liverpool Jurgen Klopp amepanga kumfanya nyota huyo wa kimataifa wa Brazil kuwa usajili wake kwanza toka akabidhiwe mikoba Anfield. Liverpool inadaiwa kuwa tayari kutoka kitita cha paundi milioni 24.5 kwa ajili ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 26. Hata hivyo, klabu hiyo ya Ukraine inamthaminisha Teixeira ambaye pia anahusishwa na tetesi za kuwindwa na Chelsea, kufikia paundi milioni 39. Klopp anataka kuimarisha safu yake ya ushambuliaji kufuatia kuumia kwa Danny Ings, Divock Origin a Daniel Sturridge.

No comments:

Post a Comment