Friday, January 1, 2016

RUFANI YA BILITY YAKATALIWA.

RAIS wa Shirikisho la Soka la Liberia, Musa Bility ameshindwa rufani yake ya kupinga kuenguliwa katika kinyang’anyiro cha urais wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA. FIFA ilimuengua Bility Novemba 12 mwaka jana katika kinyang’anyiro hicho kwa madai kuwa hakukidhi baadhi ya vigezo vya kuwa mgombea. Bility aliipinga adhabu hiyo katika Mahakama ya Kimataifa ya Michezo-CAS akitegemea jina lake kurejeshwa tena. Hata hivyo, CAS katika taarifa yake jana walitupilia mbali rufani hiyo na Bility amesema anasubiri sababu haswa za kukataliwa kwa rufani yake ili aweze kuangalia hatua zaidi za kuchukua.

No comments:

Post a Comment