Friday, January 1, 2016

VAN GAAL AWAAMBIA UNITED WASITEGEMEE MIUJIZA.

MENEJA wa Manchester United, Louis van Gaal amesema hakuna miujiza ya kuimarisha hali ya klabu hiyo zaidi ya wahusika wote kuongeza bidii. United wamecheza mechi nane bila kushinda hata moja, sita zikiwa Ligi Kuu hivyo kuwafanya kuporomoka mpaka nafasi ya sita katika msimamo. Mbali na kushuka katika msimamo pia wameng’olewa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na kuangukia katika michuano ya Europa League. Akihojiwa Van Gaal amesema hakuna miujiza, jambo muhimu wanaloweza kufanya ni kuangalia walipokosea na kuona jinsi gani wanaweza kuboresha kama timu ili waweze kupata matokeo wanayohitaji.

No comments:

Post a Comment