Thursday, February 25, 2016

AL AHLY YAMUAJIRI KOCHA WA ZAMANI WA SPURS.

MENEJA wa zamani wa Tottenham Hotspurs na Fulham, Martin Jol ameteuliwa kuwa kocha mpya wa klabu kongwe nchini Misri ya Al Ahly. Kocha huyo raia wa Uholanzi anatachukua mikoba ya Jose Peseiro wa Ureno ambaye aliondoka Januari mwaka huu kwenda kuifundisha FC Porto. Hatua hiyo inamaanisha kuwa mahasimu wa jiji la Cairo Al Ahly na Zamalek wote wameajiri makocha wapya kufuatia Zamalek wao kumchukua Alex McLeish. Al Ahly kwasasa ndio vinara wa Ligi Kuu nchini humo wakiwa juu ya Zamalek ambao ni mabingwa watetezi. Mbali na kuzinoa klabu hizo za Uingereza, Jol pia amewahi kusifundisha Humburg ya Ujerumani na Ajax Amsterdam ya Uholanzi. Jol mwenye umri wa miaka 60 amekuwa bila kibarua toka lipotimuliwa Fulham mwaka 2013.

No comments:

Post a Comment