Thursday, February 25, 2016

PELLEGRINI ASIFIA UAMUZI WAKE.

MENEJA wa Manchester City, Manuel Pellegrini amesema uamuzi wake wa kuipa kipaumbele michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya badala ya Kombe la FA umewasaidia kwa kiasi kikubwa kupata ushindi dhidi ya Dynamo Kiev jana. Pellegrini alikosolwa vikali kwa kuchezesha kikosi dhaifu katika mchezo wa Jumapili iliyopita ambao walitandikwa mabao 5-1 na Chelsea, lakini jana walifanikiwa kushinda mabao 3-1 katika mchezo wao wa mkondo wa kwanza kwa mabao 3-1. Akihojiwa Pellegrini amesema kikubwa kilichochangia kuwapumzisha nyota wake wengi katika mchezo dhidi ya Chelsea ni upungufu wa wachezaji alionao katika kikosi chake hivi sasa. Mabao ya Sergio Aguero, David Silva na Yaya Toure yalitosha kuihakikishia City ushindi huo, wakati Joe hart ambaye pia alipumzishwa katika mchezo wa FA naye alifanya kazi kubwa kuzuia mashambulizi ya Kiev.

No comments:

Post a Comment