Friday, February 26, 2016

BARCELONA KUONGEZA MKATABA NA UNICEF.

KLABU ya Barcelona imeongeza mkataba wa ushirikiano na Shirika la Kuhudumia Watoto la Umoja wa Mataifa-UNICEF ambao utadumu mpaka mwaka 2020. Katika mkataba huo mpya utashuhudia Barcelona wakichangia kiasi cha euro milioni kwa mwaka ili kuinua suala la elimu kwa watoto. Katika taarifa ya klabu hiyo iliytumwa katika mtandao imedai kiasi hicho ni ongezeko la euro nusu milioni kulinganisha na euro milioni 1.5 ambazo walikuwa wakilipa kwa mwaka katika makubaliano ya awali. Makubaliano kati ya klabu hiyo na UNICEF yalianza mwaka 2006 wakati Barcelona walipovunja utamaduni wao wa kuweka nembo mbele ya fulana zao na kuamua kuweka nembo ya UNICEF. Toka wakati huo nembo ya UNICEF imehamishwa na kuhamia nyuma ya fulana za Barcelona ili kupisha wadhamini waliotoa mamilioni ya euro ambao ni kampuni ya ndege ya Qatar. Hata hivyo, mchango wa Barcelona bado umeendelea kusaidia mamilioni ya watoto katika nchi za Ghana, China, Brazil na Afrika Kusini.

No comments:

Post a Comment