Friday, February 26, 2016

OLISEH AACHIA NGAZI SUPER EAGLES.

NAHODHA wa zamani wa timu ya taifa ya Nigeria maarufu kama Super Eagles, Sunday Oliseh amejiuzulu wadhifa wake wa ukocha w atimu hiyo. Katika baru yake aliyotuma kwa Shirikisho la Soka la Nigeria-NFF jana, Oliseh alitangaza kujiuzulu na kulishukuru shirikisho hilo kwa nafasi waliyompa ya kulitumikia taifa lake. Oliseh ambaye alichukua mikoba ya kuinoa Super Eagles Julai mwaka 2015, amekuwa na haelewani na baadhi ya viongozi wa NFF na pia wachezaji wachache. Katibu Mkuu wa NFF Dkt. Mohammed Sanusi alithibitisha kupokea barua ya kujiuzulu kwa kiungo huyo wa zamani wa Ajax Amsterdam. Hata hivyo, Sanusi amesema hawezi kwenda kwa undani kabisa kuhusiana na suala hilo kwasababu wapo katika mkutano wa uchaguzi wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA huko Zurich na pindi watakavyorudi watalishughulikia.

No comments:

Post a Comment